Thursday, February 12, 2026
spot_img
HomeBungomaUjenzi wa Uwanja wa Masinde Muliro Kanduyi unatarajiwa kukamilika kufikia mwezi Desemba...

Ujenzi wa Uwanja wa Masinde Muliro Kanduyi unatarajiwa kukamilika kufikia mwezi Desemba mwaka huu,Katibu wa wizara ya michezo Bwana Mwangi asema

Uwanja wa Masinde Muliro,Kanduyi Bungoma

Ujenzi wa Uwanja wa Masinde Muliro Kanduyi unatarajiwa kukamilika kufikia mwezi Desemba mwaka huu, kulingana na Katibu wa Wizara ya Michezo Elija Mwangi.

Mwangi aliandamana na Gavana wa Bungoma Kenneth Lusaka kukagua maendeleo ya awamu ya pili ya ujenzi huo.

Wakati wa ziara hiyo iliyohusisha maafisa kutoka serikali kuu, ilibainika kuwa kazi imefikia asilimia 94 huku shughuli za kuezeka zikiendelea.

Gavana Lusaka alielezea kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji, akimtaka mkandarasi kuongeza juhudi ili mradi ukamilike kwa wakati, akisisitiza uwajibikaji na utekelezaji kwa wakati.

Kwa upande wake, Katibu Mwangi alihakikishia wananchi kuwa serikali imejizatiti kuhakikisha uwanja huo unakamilika ndani ya muda uliowekwa na kwa viwango vinavyokubalika, akiongeza kuwa hakutakuwa na nafasi ya uzembe wala ubora hafifu.

Viongozi hao walieleza matumaini kwamba uwanja huo utakapoanza kutumika, utaimarisha michezo, kukuza vipaji vya vijana na kuchangia ukuaji wa uchumi katika Kaunti ya Bungoma.

RELATED ARTICLES

1 COMMENT

  1. I like the helpful info you provide in your articles. I will bookmark your weblog and check
    again here regularly. I am quite certain I will learn many
    new stuff right here! Good luck for the next!

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
Google search engine

Most Popular

Recent Comments

soumis on
Rhys on
WooCommerce on
WooCommerce on
WooCommerce on
WooCommerce on
WooCommerce on
Open chat
Chat On WhatsApp!
Hello
Can we help you?