Uwanja wa Masinde Muliro,Kanduyi Bungoma
Ujenzi wa Uwanja wa Masinde Muliro Kanduyi unatarajiwa kukamilika kufikia mwezi Desemba mwaka huu, kulingana na Katibu wa Wizara ya Michezo Elija Mwangi.
Mwangi aliandamana na Gavana wa Bungoma Kenneth Lusaka kukagua maendeleo ya awamu ya pili ya ujenzi huo.
Wakati wa ziara hiyo iliyohusisha maafisa kutoka serikali kuu, ilibainika kuwa kazi imefikia asilimia 94 huku shughuli za kuezeka zikiendelea.
Gavana Lusaka alielezea kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji, akimtaka mkandarasi kuongeza juhudi ili mradi ukamilike kwa wakati, akisisitiza uwajibikaji na utekelezaji kwa wakati.
Kwa upande wake, Katibu Mwangi alihakikishia wananchi kuwa serikali imejizatiti kuhakikisha uwanja huo unakamilika ndani ya muda uliowekwa na kwa viwango vinavyokubalika, akiongeza kuwa hakutakuwa na nafasi ya uzembe wala ubora hafifu.
Viongozi hao walieleza matumaini kwamba uwanja huo utakapoanza kutumika, utaimarisha michezo, kukuza vipaji vya vijana na kuchangia ukuaji wa uchumi katika Kaunti ya Bungoma.




I like the helpful info you provide in your articles. I will bookmark your weblog and check
again here regularly. I am quite certain I will learn many
new stuff right here! Good luck for the next!