Naibu chifu wa kata ndogo ya Aterait katika eneo bunge la Teso kusini Edwin Anyiko amenusurika kifo usiku wa kuamkia leo, baada ya watu wasiojulikana kuteketeza nyumba yake usiku wa kuamkia leo.Naibu chifu huyo ambaye ana miezi 5 afisini, anadai yuko hatarini baada ya juhudi zake za kupambana na pombe haramu na wizi wa mifugo eneo hilo kupata pingamizi kutoka kwa baadhi ya wenyeji.



